23 Quotes by Enock Maregesi about Jesus







  • Author Enock Maregesi
  • Quote

    Watakatifu wote watanyanyuliwa na wataondoka pamoja na Yesu kuelekea mbinguni, kwa ajili ya ziara ya miaka 1000 katika ulimwengu wa roho; kuanzia dunia ya kwanza ya ulimwengu huo iitwayo Asiyah hadi ya mwisho iitwayo Adam Kadmon, katika mji mpya wa Yerusalemu.Baada ya milenia, kipindi hicho huku duniani Ibilisi akiwa kifungoni na malaika wake, binadamu wote wenye dhambi wakiwa wamekufa, Yesu na watakatifu wote atarudi kwa ajili ya ufufuo wa pili; na kama mfalme wa ulimwengu wote milele.

  • Tags
  • Share

  • Author Enock Maregesi
  • Quote

    Unaweza kuwa umeomba kuhusu jambo fulani kwa muda mrefu bila majibu, lakini siku moja ghafla ukajibiwa wakati umejisahau. Kwa nini? Kwa sababu Mungu hufanya kazi zake kwa siri. Ukiomba jambo kutoka kwa Mungu, huku ukiwa huna kinyongo na mtu yeyote na bila moyo wako kusita wakati ukiomba, tambua katika moyo wako kwamba tayari umeshajibiwa. Kisha lipotezee, hilo jambo, kila siku, usiwe unalikumbukakumbuka, hadi Mungu mwenyewe atakapokujibu. Hata Yesu atakaporudi kila mtu atakuwa amejisahau.

  • Tags
  • Share

  • Author Enock Maregesi
  • Quote

    Kuna watoto wa Mungu na kuna watoto watakatifu wa Mungu. Watoto wa Mungu ni wale waliobatizwa na kumkaribisha Kristo kama kiongozi wa maisha yao, na hata wale ambao hawajabatizwa na kumkaribisha Yesu kama kiongozi wa maisha yao kwa maana ya uumbaji, wakati watoto watakatifu wa Mungu ni mitume na manabii wa kweli.

  • Tags
  • Share