4 Quotes by Enock Maregesi about almighty-god
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Akili yako isipokuwa timamu, familia itakushinda. Familia ikikushinda utalaumiwa na Mwenyezi Mungu.
- Tags
- Share
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Mheshimu sana mtu aliyekupandisha juu kwa sababu utakaposhuka ndiye atakayekupokea, ijapokuwa unaweza usishuke kabisa au unaweza kushuka ukapokelewa na mtu mwingine baki, kwa kudura za Mwenyezi Mungu.
- Tags
- Share
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Mtu akikuita mjinga au mpumbavu juu ya maisha yako usikasirike kwa sababu wewe si mjinga wala mpumbavu. Sema hapana kwa ndiyo nyingi kwa sababu hawapaswi kuingilia mambo ya mtu mwingine bila idhini ya Mwenyezi Mungu. Kuingilia mambo ya mtu mwingine bila idhini ya Mwenyezi Mungu ni dhambi, tena dhambi kubwa, ni kuvunja amri kuu ya kwanza ya Mungu.
- Tags
- Share
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Matatizo ya kijamii, kimiiko, kimaadili, kisiasa, na kiroho; hayataweza kutatuliwa kwa pesa, vikao vya kifamilia, haki za binadamu, usalama wa taifa, au nguvu za kijeshi. Yataweza kutatuliwa kwa haki na hekima ya Mwenyezi Mungu.
- Tags
- Share