922 Quotes by Enock Maregesi

  • Author Enock Maregesi
  • Quote

    Kama miaka 1000 ya duniani ni sawa na siku moja ya Mungu; hivyo basi, miaka 930 aliyoishi Adamu ni sawa na siku 0.93 au saa 22:32 za Mungu. Kwa hiyo, ili siku ya Mungu itimie Adamu alipaswa kuishi miaka 70 (siku 0.07 au saa 1:68) zaidi! Ukiidadavua saa 1:68 unapata saa 2:08. Kulingana na muda wa mbinguni tunapaswa kuishi kwa muda wa saa 2:08! Muda huo ni mfupi sana.

  • Tags
  • Share

  • Author Enock Maregesi
  • Quote

    Mpelelezi wa Tume ya Dunia kutoka Jerusalem, Israeli, Kanali Daniel 'Yehuda Ben-Asher' Ebenezer, Daniel Yehuda, alikuwa komandoo wa kitengo cha mauti na utekaji nyara cha Shirika la Kijasusi la Mossad la Israeli (Kidon) kabla ya kujiunga na Kikosi Maalumu cha Kikomandoo cha Tume ya Dunia (EAC) huko Oslo, kwa makubaliano maalumu kati ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (UNSC) na Shirika la Kijasusi la Mossad la Israeli.

  • Tags
  • Share

  • Author Enock Maregesi
  • Quote

    Mungu anataka tujifunike kwa ngao yake. Yaani, tuwe na imani iliyokomaa katika Bwana na yeye atatufunika. Maana ya kauli hiyo ni kwamba kila kiungo cha miili yetu kuanzia unyayo hadi kichwa lazima kifunikwe kwa silaha ya Mungu, ambayo Mungu anaiita panoplia. Panoplia haimo katika kamusi ya Kiswahili au Kiingereza, lakini maana yake ni ‘ngao kamili ya Mungu’. Hii si tu silaha ya Mungu. Ni silaha kamili ya Mungu tunayotakiwa kujifunika kwayo.

  • Tags
  • Share



  • Author Enock Maregesi
  • Quote

    Heshimu kila mtu. Ongea na kila mtu. Msikilize kwa makini kila unayeongea naye. Maana Mungu anaweza kumtumia mtu yeyote, hata kichaa, kukupa ufunuo wa mambo yake.

  • Tags
  • Share