15 Quotes by Enock Maregesi about Evil
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Uovu ni aibu kwa taifa zima!
- Tags
- Share
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Wachawi wanaabudu miungu ambayo ndani yake kuna Shetani, aliyesababisha Ibilisi achague mabaya badala ya mema kabla Mungu hajamfukuza mbinguni. Shetani ndani yake kuna Shetani. Huyo Shetani aliyeko ndani ya Shetani, anayeitwa Roho ya Mabadiliko ya Kweli ya Ufahamu Kamili wa Siri ya Uumbaji wa Mungu (kwani ukiijua siri ya uumbaji wa Mungu unakuwa kama Mungu), ndiye anayeabudiwa na wachawi.
- Tags
- Share
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Nguvu za hasi ni mawazo mabaya, na nguvu za chanya ni mawazo mazuri. Nguvu za hasi ni Shetani, kwa vile Shetani ndiye anayeleta mabaya. Nguvu za chanya ni Mungu, kwa vile Mungu ndiye anayeleta mazuri. Katika dunia hii utapambana na Shetani lakini hutamshinda, kwani hapa ndipo anapotawala. Pambana na Shetani katika dunia ya kiroho, kwa maana ya maombi na utiifu kamili kwa Mwenyezi Mungu, kama unataka kuzishinda nguvu zake.
- Tags
- Share
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Mungu hakutuumba ili tuwe roboti, ambayo hufanya kazi kama ilivyoelekezwa. Alituumba ili tuwe huru. Yaani, tuwe na uwezo wa kuchagua mema au mabaya – ndiyo maana akaweka Mti wa Maarifa ya Mema na Mabaya katika Bustani ya Edeni – ndiyo maana akamtuma Shetani kuwajaribu Adamu na Hawa, wazazi wetu wa kwanza.
- Tags
- Share
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Hakuna mtu mwenye akili timamu anayetaka mabaya katika maisha yake. Mwanamume atake mwanamke mwenye matendo mema. Mwanamke atake mwanamume mwenye matendo mema. Misingi ya hasanati ni misingi ya utu. Tukiishi katika misingi ya utu, misingi ya matendo mema, tutaishi sawasawa na mapenzi ya Mungu. Kila mtu anapaswa kuishi na mke au mume aliye mwema.
- Tags
- Share
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Kama nje ya uwezo wa kisheria ni uovu, hivyo basi, ndani ya uwezo wa kisheria ni wema. Kila mtu amepewa vipaji na Mwenyezi Mungu. Tumia vipaji vyako kutenda mema. Usitumie vipaji vyako kutenda maovu.
- Tags
- Share