84 Quotes by Enock Maregesi about people
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Falsafa ya Usawa kwa Watu na Vitu Vyote ya Yin-Yang ya Kichina ni falsafa inayotumiwa na Wachina, kujifunza sanaa ya mapigano na kutengeneza madawa ya asili, na magaidi wa madawa ya kulevya wa Amerika ya Kusini na Kaskazini kusaidia watu waliosahauliwa na serikali zao.
- Tags
- Share
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Kila mmoja wetu ana kitu cha kutoa. Wengine wana pesa, wengine wana vipaji, wengine wana muda. Vipaji vyote tulivyopewa na Mungu, vikubwa au vidogo, hatuna budi kuvitumia kiukarimu kwa watu wanaovihitaji. Tunapofanya hivyo tunaleta mabadiliko katika dunia kwa ajili ya watu fulani, na tunapata maana halisi ya maisha na toshelezo la moyo katika maisha yetu.
- Tags
- Share
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Isipite siku hata moja katika maisha yako bila kusema hata kimoyomoyo kwa wazazi wako na kwa watu wote wanaokupenda kwamba unawapenda, kwani siku moja hawatakuwepo tena.
- Tags
- Share
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Afrika isomeshe watu wake, na itumie vizuri mapato yanayotokana na mauzo ya rasilimali zake kwa faida ya jumla ya wananchi wa nchi zake, kusudi baadaye wawe wataalamu wa rasilimali za nchi zao wenyewe, kuepukana na utumwa wa rasilimali. Rasilimali za Afrika zina miiko na masharti yake.
- Tags
- Share
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Mungu akikubariki kipaji chako watu watasema ni laana. Maisha yako ni sawa na mto. Unakoelekea ni baharini. Lakini sasa umefika kwenye mlango wa bahari. Unahangaika upite wapi kufika baharini, ambapo utaogelea kwa kadiri utakavyoweza. Utakapofika baharini, watu, badala ya kusema umebarikiwa, watasema umelaaniwa, badala ya kukuita malaika, watakuita shetani. Mafanikio hayapimwi kwa pesa au mali kiasi gani unayo, mafanikio yanapimwa kwa amani ya moyo au maisha ya watu kiasi gani umeboresha.
- Tags
- Share
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Neno moja kutoka mdomoni mwako linaweza kukuletea madhara makubwa. Waweza kusema kitu ukadhani umepatia kumbe umeharibu. Fikiria kwanza maana ya kitu unachosema, halafu sema.
- Tags
- Share
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Kuwa mwangalifu unapoongea na watu. Huwajui!
- Tags
- Share
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Kiongozi wa wananchi au wa serikali hapaswi kuchaguliwa au kuteuliwa kwa ajili ya kupata sifa ya madaraka na hivyo kunyanyasa na kudharau watu kwa sababu ya madaraka yake, anapaswa kuchaguliwa au kuteuliwa kwa ajili ya kuleta mabadiliko katika nchi kama kiongozi wa dhima aliyokabidhiwa kwa unyenyekevu na heshima kwa wananchi wenzake.
- Tags
- Share
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Kutunza siri wakati mwingine ni kitu kigumu sana kwa baadhi ya watu lakini watu wanapaswa kuwa na uwezo wa kutunza siri kujijengea uaminifu, ambao ni siri ya mafanikio.
- Tags
- Share