76 Quotes About Maisha
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Mwambie mtoto wako maneno mazuri anapokuwa ananyonya na kukuangalia machoni kwa kukukodolea. Maneno utakayomwambia ndiyo yatakayokuwa msingi wa mawazo yake, na ndiyo yatakayoumba maisha yake atakapokuwa mkubwa.
- Tags
- Share
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Mahatma Gandhi alipigwa risasi na kufariki dunia baada ya maisha yake kumfelisha. Lakini kifo chake kiliipatia India uhuru kutoka Uingereza. Hivyo, akafanikiwa.
- Tags
- Share
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Wakati ndege inapaa huwa inapambana na upepo. Lakini inapaa, hata hivyo.
- Tags
- Share
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Mungu akikubariki kipaji chako watu watasema ni laana. Maisha yako ni sawa na mto. Unakoelekea ni baharini. Lakini sasa umefika kwenye mlango wa bahari. Unahangaika upite wapi kufika baharini, ambapo utaogelea kwa kadiri utakavyoweza. Utakapofika baharini, watu, badala ya kusema umebarikiwa, watasema umelaaniwa, badala ya kukuita malaika, watakuita shetani. Mafanikio hayapimwi kwa pesa au mali kiasi gani unayo, mafanikio yanapimwa kwa amani ya moyo au maisha ya watu kiasi gani umeboresha.
- Tags
- Share
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Mungu akikuweka mahali unapostahili kuwa, kulingana na takdiri ya maisha yako, hakuna mtu mwenye uwezo wa kushindana na kipaji chako.
- Tags
- Share
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Ningependa – maisha yangu yatakapokoma hapa duniani – kukumbukwa kama mtu aliyejitahidi kwa kadiri ya uwezo wake wote, kutumia kipaji alichopewa na Mungu.
- Tags
- Share
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Wazazi wetu ni watu wa kuheshimu kuliko kitu kingine chochote kile kwa sababu wana uwezo wa kuona tusipoweza kuona. Yaani, wanajua kilichokuwepo kabla ya sisi kuzaliwa na wanajua kilichokuwepo baada ya sisi kuzaliwa. Maisha tuliyopitia, wazazi wetu walishapitia. Tulipokuwa, wazazi wetu walishakuwepo; na tulichofanya, wazazi wetu walishafanya. Hivyo, hatuna budi kuwaheshimu wazazi wetu. Lakini, wazazi wetu wanapaswa kujiheshimu kutufundisha adabu na maadili mema.
- Tags
- Share
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Maisha yangu ni darasa. Jifunzeni kutokana na maisha yangu, jifunzeni kutokana na sifa zangu za ushupavu, jifunzeni kutokana na sifa zangu za udhaifu, kutatua matatizo katika maisha yenu.
- Tags
- Share
- Author Enock Maregesi
-
Quote
Yesu Kristo alilipa gharama ya maisha yake kutununua kutoka kwa Shetani. Alijitolea maisha yake ili wengine waweze kuishi. Upendwe vipi?
- Tags
- Share