10 Quotes by Enock Maregesi about leader

  • Author Enock Maregesi
  • Quote

    Kuna watoto wa Mungu na kuna watoto watakatifu wa Mungu. Watoto wa Mungu ni wale waliobatizwa na kumkaribisha Kristo kama kiongozi wa maisha yao, na hata wale ambao hawajabatizwa na kumkaribisha Yesu kama kiongozi wa maisha yao kwa maana ya uumbaji, wakati watoto watakatifu wa Mungu ni mitume na manabii wa kweli.

  • Tags
  • Share



  • Author Enock Maregesi
  • Quote

    If a leader for the right reasons is blessed by God, even the people he leads will be blessed by God as well. But if the leader is cursed by God because of iniquity, even the people he leads will be cursed as well.

  • Tags
  • Share




  • Author Enock Maregesi
  • Quote

    Katika maisha, kila mtu ni kiongozi na ni mfuasi pia kutegemeana na hali. Kiongozi hatakiwi kuwa na kiburi, wala hatakiwi kuwa na roho yenye kutakabari, roho ya jeuri na kuona wengine si kitu, kwa sababu kiburi na roho yenye kutakabari huleta maangamizi na maanguko makubwa katika jamii. Viongozi wa mataifa wana jukumu kubwa kwa sababu kama wataruhusu maadili yaanguke, nguvu zao zote za kijeshi na kiteknolojia hazitawasaidia. Sifa ya kwanza ya kiongozi ni kuwa na maadili mema.

  • Tags
  • Share

  • Author Enock Maregesi
  • Quote

    Kura ni haki yako ya msingi kabisa kwa ajili ya maendeleo yako na ya nchi yako. Ongea na nchi yako. Yaani, chagua kiongozi atakayeweza kukuletea maendeleo. Kama hujachagua mtu, usimlalamikie yule aliyechaguliwa.

  • Tags
  • Share