43 Quotes About Mtu




  • Author Enock Maregesi
  • Quote

    Boresha maisha ya watu kwa kadiri utakavyoweza. Ukisaidia mtu 1 watahurumiwa watu 10. Ukisaidia watu 10 watahurumiwa watu 100. Ukisaidia watu 100 watahurumiwa watu 1000. Kila mmoja wetu akitambua wajibu wake katika jamii, Mungu atatuhurumia sisi wote. Maisha ya mtu mmoja yakiboreka, mmoja huyo ataboresha na ya wengine wengi. Hivyo, endelea kuogelea lakini usisahau kurudi nyuma katika jamii.

  • Tags
  • Share


  • Author Enock Maregesi
  • Quote

    Usimdharau mtu aliyesaidia kukusukuma juu katika ngazi ya mafanikio yako, ikiwa utafanikiwa, kwa sababu kuna leo na kesho. Ukishuka, kama ulimdharau, hatakuamini tena. Lakini ukishuka, kama ulimheshimu, na kama bado ana uwezo wa kukupandisha juu, atakupandisha tena.

  • Tags
  • Share